0


MANCHESTER, ENGLAND
RUUD VAN NISTLEROOY (PIichani chini) kumbe alionyeshwa mlango wa kutokea Manchester United baada ya  kutofautiana na Cristiano Ronaldo mara tu alitoa maoni yake kufuatia kifo cha baba wa staa huyo wa Ureno.
Awali Mholanzi huyo alikuwa kipenzi cha Old Trafford, lakini alionyeshwa mlango wa kutokea muda mfupi baada ya kutaka kushindana na Ronaldo kitendo kilichomfanya Kocha Sir Alex Ferguson kutokuwa na uamuzi mwingine zaidi ya kumuondoa kikosini.
Sababu ya kuondolewa kwa Van Nistlerooy imeandikwa katika kitabu kilichochapishwa hivi karibuni na bosi wa Mawasiliano wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair, Alastair Campbell ambaye ni rafiki wa karibu wa Sir Alex Ferguson.
Kama alivyonukuriwa na Gazeti la Times, Campbell alionyesha ni kwa kiasi ilikuwa vigumu kumuongoza Van Nistlerooy kwa kuwa alikuwa mbinafsi, na kumfanya Ferguson kutokuwa na cha kufanya juu ya mchezaji huyo.
“Ukorofi wa mwisho aliufanya pale alipomwambia Cristiano Ronaldo amepata baba mpya ambaye ni Carlos (Queiroz, aliyekuwa kocha msaidizi wa Ferguson) mara baada ya baba wa Ronaldo, kufafiriki kutokana na unywaji wa pombe,” aliandika Campbell.

“Carlos alimtaka Van Nistlerooy kuonyesha heshina na akajibu hamuheshimu mtu yeyote pale. Hatimaye aliomba radhi lakini Ronaldo hakumkubalia.

    Ronaldo akiwa na Carlos Queiroz walipokuwa United.
 “Alex (Ferguson) alimrudisha Van Nistlerooy nyumbani pindi aliposikia kuhusu hilo. Lakini hakuwa na uhakika alichotaka kufanya juu yake,” Campbell aliongeza.
Katika majira ya joto, Van Nistlerooy alionyeshwa mlango wa kutoka Old Trafford na kuuzwa kwa miamba ya Hispania, Real Madrid. 

                    Campbell akiwa na Ferguson.
Straika huyo wa Kiholanzi  aliifungia United jumla ya mabao 95 katika Ligi Kuu England katika michezo 150 aliyocheza. 


Post a Comment

 
Top