STOKE,
ENGLAND
JORDAN Ibe ameifungia Livapool bao la pekee
katika mchezo wa fainal ya kwanza ya Kombe la Capital One jana Jumanne dhidi ya
Stoke lakini wachezaji wa timu hiyo wamelala na viatu.
Kocha
wa Liverpool, Jurgen Klopp aliingiwa na
wasiwasi baada ya wachezaji wake watatu kuumia nyama za nyuma ya paja katika Uwanja wa Britannia.
Kiungo Coutinho akiugulia maumivu
Philippe
Coutinho na Dejan Lovren walilazimika kutoka
katika kipindi cha kwanza wakati
beki Kolo Toure alicheza baada ya kufungwa bandeji katika dakika za lala
salama.
Coutinho
alilazimika kutoka dakika ya 18 na nafasi yake kuchukuliwa na mfunguji wa bao
hilo, Ibe.
Beki Lovren akiugulia
Kocha
Klopp alichanganyikiwa zaidi baada ya
beki wake Lovren kuumia katika kipindi hicho
cha kwanza.
Toure
alionekana kuwa mchezaji wa tatu kupatwa na majeraha hayo lakini Mu-ivory Coast huyo alicheza akiwa na
maumivu katika dakikia hizo za majeruhi.
Coutinho
na Lovren ambaye nafasi yake ilichukuliwa na James Milner katika dakika ya 34, watakuwa nje kwa
kipindi kirefu cha matibabu wakati timu yao ikiwa inakabiliwa na michezo migumu
ya Ligi Kuu dhidi ya Arsenal na Manchester United hivi karibuni.
Beki Kolo Toure naye akiugulia maumivu
Wachezaji
hao wamejiunga na Daniel
Strirridge (anadaiwa atarudi hivi karibuni), Jordan Henderson, Martin Skrtel.
wengine ni Joe Gomez (goti), Jon Flanagan (goti), Mamadou Sakho (goti), , Jordan Henderson (kisigino), Jordan Rossiter (misuli ya paja), Danny Ings (goti), na Divock Origi (misuli ya paja).
wengine ni Joe Gomez (goti), Jon Flanagan (goti), Mamadou Sakho (goti), , Jordan Henderson (kisigino), Jordan Rossiter (misuli ya paja), Danny Ings (goti), na Divock Origi (misuli ya paja).
Post a Comment